Advertisements

Friday, May 27, 2016

DADA WA BILIONEA MSUYA AUAWA KWA KUCHINJWA

Marehemu Aneth Msuya wakati wa uhai wake 

By Daniel Mjema, Mwananchi dmjema@mwananchi.co.tz

Moshi. Mtumishi wa Wizara ya Fedha, Aneth Msuya (30) ambaye ni mdogo wa Bilionea Erasto Msuya, ameuawa kwa kuchinjwa nyumbani kwake eneo la Kigamboni jijini Dar Es Salaam.

Akizungumza na mwandishi wa habari hii kwa simu kutoka Mererani, mmoja wa ndugu wa familia hiyo, Shujaa Khamis, alithibitisha kuuawa kwa Aneth (pichani), lakini alikataa kuingia kwa undani.

“Ni kweli wamemchinja usiku wa kuamkia leo (jana) na hapa nipo kwenye msiba hapa nyumbani (Mererani) kwa baba. Tumeambiwa wamechukua Tv tu,” alisema.

Hata hivyo, Khamis alikataa kueleza lolote kama wana mashaka na mauaji hayo zaidi ya kuliomba Jeshi la Polisi nchini, kuchunguza kiini cha mauaji hayo na kuwasaka waliohusika.

Habari nyingine kutoka Wizara ya Fedha, ziliwakariri baadhi ya watumishi wakisema wamepata taarifa za msiba huo, lakini hawajapewa taarifa rasmi.

“Tuna taarifa tunazisikia sikia kuwa ameauawa, lakini jana (juzi) tulikuwa naye kazini ila leo (jana) ndiyo tunasikia amechinjwa na watu wasiojulikana. Imetusikitisha sana,” alisema mmoja wa watumishi hao ambaye hakutaja jina kwa kuwa si msemaji.

Kamanda wa mkoa wa Kipolisi wa Temeke, Andrew Satta alipofutwa jana kuthibitisha taarifa za mauaji hayo alisema yuko kwenye kikao, na kuomba atafutwa baadaye akiwa sehemu nzuri ya kuongea.

1 comment:

Anonymous said...

Jamani...R.i.p dada