Advertisements

Friday, May 27, 2016

CHUMBA CHA DEREVA TAX CHAZUA KIZAA ZAA MTAA WA MBEZI MTONI GOLD STAR, DAR

Sehemu ya tahamani za ndani za Dereva huyo, Feni na Kabati zilizokutwa ndani ya chumba hicho, pamoja na Chupa za plastiki zilizojaa mokojo, nguo zake juu ya chupa hizo.

Na Ripota wa Sufianimafoto Blog, Dar

UKIHADITHIWA na kuonyeshwa chumba cha Dereva Tax anayeonekana kitaani na katika kazi zake akiwa amepiga pamba wala hutaamini masikio yako wala macho yako pindi utakapopata bahati ya kufika na kushuhudia chumba hicho kilichopo maeneo ya Gold Star Mtaa wa Mbezi Mtoni Bondeni jijini Dar es Salaam.
Mtandao huu ulipata fursa ya kufika na kushuhudia yale yaliyokuwa yakisemwa na baadhi ya wakazi wa mtaa huo jana majira ya saa tano usiku baada ya kutokea mtafaruku na sintofahamu katika nyumba hiyo ya Mama Mwakajinga, anayoishi Dereva huyo aliyejulikana kwa jina la Steven al-maarufu kama 'NYATI'.
Akizungumza na mtandao huu wa Sufianimafoto, Mama mwenye nyumba kuhusu tukio hilo, alisema kuwa siku ya Mei 23, akiwa ameketi uwanji karibu kabisa na Chumba cha Jamaa huyo huku akichambua mboga, alihisi harufu kali na mbaya iliyokuwa ikivuma kutoka chumbani kwa Dereva huyo aliyepanga katika nyumba yake tangu mwaka 2008 na kuona wadudu aina ya funza wakitoka chumba hicho kupitia chini ya mlango.
Godoro la Dereva huyo ambapo ndiyo mahala anapopumzika pindi atokapo kazini.
Kesho yake Mei 24 Baada ya kuona wadudu hao huku harufu ikizidi kuwa kali, alimuita jirani yake na kumshirikisha jambo hilo huku wote wakishikwa na butwaa na kuwa na mashaka na chumba hicho.

Mei 25 Mama mwenye nyumba aliamua kwenda kwa Mjumbe wa eneo hilo Badili Makoye, kutoa taarifa juu ya wasiwasi uliotanda katika nyumba hiyo na kuongozana na Viongozi wengine, Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa huo, Frank Kyaruzi, Wajumbe wengine Abdalla Mlaliya na Matrida Paston, waliofika na kujionea hali halisi ya chumba hicho.
Mama Mwenye nyumba, akifungua mlango wa chumba cha mpangaji wake huku baadhi ya wakazi wa eneo hilo wakishuhudia.

Baada ya viongozi hao kufika eneola tukio walimuamuru Mama mwenye nyumba kwenda kutoa taarifa kituo cha Polisi. Mama huyo alitekeleza agizo na kwenda kuripoti Kituo cha Mbezi Garden na kuongozana na Mkuu wa Kituo hicho na baadhi ya askari hadi nyumbani na kukuta hali hiyo ya sintofahamu.
Mama mwenye nyumba,akionesha uchafu uliokutwa chumbani humo.

Walipofika eneo la tukio na kushuhudia hali hiyo, Mkuu wa Kituo aliamuru mlango huo uvunjwe huku wanachi na Viongozi wa Mtaa huo wakishuhudia na kuingia ndani ambako walikuta Chumba kizima kikiwa kimejaa Chupa za Plastiki zilizojaa mikojo, Mifuko ya Rambo ikiwa na Vinyesi, Feni moja iliyochomekwa kwenye Soketi ya Umeme ukutani, Pakiti nyingi tupu za Sigara aina ya Embassy na Kondomu zilizotumika na zisizotumika.
Mashuhuda wakiwa nje ya nyumba hiyo wakati wa zoezi hilo la kufungua chumba hicho.

Baada ya zoezi hilo, Mwenyenyumba alimpigia simu mpangaji wake na kumtaka kurejea nyumbani, lakini Dereva huyo alijibu kuwa kwa muda huo alikuwa mbali maeneo ya Kunduchi na kuahidi kuwagongea usiku pindi atakaporejea.

Hadi Mtandao huu unaondoka eneo la tukio majira ya saa tano usiku bado wakazi wa maeneo hayo walikuwa wamejazana nje ya Chumba hicho wakiendelea kumsubiri arudi ili kupata ukweli kuhusu mambo waliyoyaona katika chumba chake.
Baadhi ya majiraji wakiangalia Albam la Dereva huyo,lililokutwa chumbani humo.

Aidha Mama mwenye nyumba aliuambia mtandao huu kuwa mpangaji wake huyo, tangu alipohamia katika nyumba hiyo mwaka 2008, hakuwahi kumuona akiingia na mwanamke katika chumba hicho, wala kumuona mgeni wa aina yeyote kwa Dereva huyo,jambo lililomshangaza kukuta Kondom zilizotumika katika chumba hicho. Ama kweli ukistaajabu ya Mussa utayaona ya Filauun.
Majirani wakipekua begi lililokutwa katika chumba hicho.

Hadi leo hii Mei 27, mtandao huu umeshindwa kumpata dereva huyo baada ya kutompata hewani simu yake ikiwa imezimwa tangu kutokea kwa tukio hilo. 

Leo hii Mei 27, Mama mwenye nyumba ameripoti kuwa mpangaji wake huyo,hajatokea nyumbani hapo tangu kutokea kwa tukio hilo ambapo leo, amechukua uamuzi wakuwalipa vijana wa mtaa huo ili wasafishe chumba hicho.

Tayari tumewalipa pesa vijana kiasi cha sh.200,000/= ili wafanya usafi na wameshamaliza na kwenda kufukia bonde la mto Mbezi.
Mashuhuda wakiwa nje ya nyumba hiyo
Mjumbe Abdallah Mlali (kushoto) akiwa na mama mwenye nyumba na majirani wakionesha uchafu huo.
Mjumbe wa Mtaa huo, Badili Makoye (wa pili kulia) akiwa na Mama mwenye nyumba na baadhi ya majirani.
Pakiti za sigara zikionekana baada ya kukunja godoro.
CHUMBA CHA DEREVA TAX, KWELI BALAAAAAAA

1 comment:

Anonymous said...

Mmmmh! Mgonjwa wa akili huyu!