Na Mwandishi Wetu
ASKARI wa Kikosi
cha Polisi cha Usalama barabarani, Kituo cha Polisi Mlandizi wamewasotesha kwa
takribani masaa mawili na nusu wanahabari kupata risiti
ya malipo ya faini aliyotozwa dereva wao baada ya kudaiwa kufanya
kosa la kutaka kulipita
gari lingine sehemu isiyoruhusiwa.
Sakata hilo
lilianza wakati polisi alipolisimamisha gari hilo katika Kituo cha Visiga, Mlandizi, wilayani Kibaha, Pwani ambapo
alimuomba dereva leseni yake na kumuamuru ateremke ili ajieleze akiwa nje ya
gari na hatimaye kumlipisha faini ya sh. 30,000 kwa kosa hilo.
Baada ya
wanahabari waliokuwa kwenye gari hilo kumsubiri dereva kwa takribani nusu saa,
waliamua kuteremka kumfuata kujua kinachoendelea, kwani wana haraka ya kufika
Dodoma muda waliopangiwa ili waungane na msafara wa Katibu Mkuu wa CCM,
Abdulrahman Kinana kwenda Singida kwenye maadhimisho ya miaka 39 ya kuzaliwa
CCM.
Lakini baada ya
mmoja wao kuwauliza Trafiki sababu zinazosababisha kutomwachia dereva, walijibu
kwa kashfa na kejeli, wakihoji kwani nyie ni akina nani? na dereva wenu
asipolipa faini basi watakaa hapo kituoni hadi jioni.
Mmoja wa
wanahabari hao alilipa faini ya sh. 30,000 na kuomba risiti. Hapo ndo
songombingo ilianza ambapo Trafiki wa kike alijibu kuwa hawana risti bali
kinachofanyika pale ni kuandikiwa tu taarifa ya kosa lao na kwenda
Kituo cha Polisi
cha Mlandizi kilichopo takribani umbali wa Km 5, na wengine waliokamatwa kwa
makosa mbalimbali ya usalama barabarani waliamuliwa kwenda kupata risiti katika
kituo hicho.
Mabishano makubwa
yalitokea hapo baina ya Trafiki na wanahabari waliokuwa wanahoji ni kwa nini
kitabu cha risiti wala mashine za kielekroniki havipo hapo ili kurahisisha
kazi. Askari wa kike na mmoja wa kiume walijibu kuwa wasifundishwe kazi.
"Msitupotezee
muda hapa, nendeni Mlandizi, mkapate hiyo risiti,"alisema trafiki wa kike.
Wakati anasema hivyo kumbe mhasibu wao alikuwepo palepale Visiga, lakini bila
kuwaambia ondokeni naye ili akawahudumie."
Pia, mmoja wa
Trafiki aliuponda sana utaratibu wa wakosaji kulipia faini kwa kutumia mashine
za elekroniki akidai kwamba ni hasara kwa trafiki na madereva ni bora mashine
hizo ziishie Dar es Salaam zisipelekwe Mkoa wa Pwani.Trafiki
wengine walisikika wakisema
kuwa hivi hawa jamaa wanaolazimisha kupewa risiti ni akina nani, waache waende
zao, wakafie mbali.
Maneno hayo
yalionekana kuwaudhi wanahabari na kuamua kuondoka kwenda Kituo cha Polisi
Mlandizi, kufuatilia risiti, lakini walichokikuta huko ni maajabu, hasa ya
kuambiwa kuwa Mhasibu hayupo ofisini kwake amekwenda kununua peni.
Baada ya
wanahabari hao kusubiri kwa takribani saa moja, waliamua kwenda kaunta kuulizia
na kuomba kuzungumza na Mkuu wa Kituo ili awasaidie kupata risiti wawahi kwenda
Dodoma, lakini mmoja wa askari aliyekuwa zamu aliwajibu kuwa Mkuu wa Kituo
hajafika ofisini amepitia Kibaha Mjini kwenye mkutano.
Alipoombwa
awasaidie kumpata mhasibu, askari huyo alitoka nje hadi ofisi ya Mhasibu
alipomkosa akaamua kumpigia simu na kuwajibu kuwa ametoka mara moja kwenda
kununua peni. Jambo hilo liliwashangaza sana wanahabari na kuanza kuhoji kwamba
iweje kitendo cha kununua peni kitumie muda wote huo na kusababisha watu
wakiwemo wao kukosa huduma tena asubuhi majira ya saa 3?
Mmoja wa wananchi
aliyekwenda kituoni kupata huduma ya risiti, alisikika akilalamika kuwa tabia
hiyo ya kuchelewesha kutoa huduma ipo sana kituoni
hapo na kwamba wanaoonekana kabisa hawaendani na kasi ya kufanya
kazi anayoitaka Rais Dk John Magufuli ya 'Hapa Kazi Tu'.
Mle ndani ya Kituo
cha Polisi walisikika wakiulizana kwamba hivi hawa watu wanaowasumbua na kutaka
kuzungumza na mkuu wa kituo ni akina nani hawa, eti wanataka risiti, ebu
tumpigie simu mhasibu aje atuondolee balaa hapa.
Baada ya muda
askari mwenye E 3275 alitoka nje na kuwaambia wanahabari kuwa mhasibu amepigiwa
simu atakuja muda si mrefu mhudumiwe muondoke, lakini mmoja wa wanahabari hao
anayemiliki blogu ya Full Shangwe, John Bukuku, alihoji kuwa hivi ni
kwanini polisi wa kituo hicho hawaendani na kasi ya Rais Dk. Magufuli? alijibu
kuwa kwani kuna nini?
Baada ya muda
Mhasibu aliwasili kwa Bodaboda, na alipofika aliwakebehi
wanahabari kwamba
anawashangaa kwa yeye kumuacha kule Visiga
alikokuwa nao na
kuwahi kituoni, ndipo wanahabari nao wakashangaa kumuona tena kituoni hapo
wakati wlipofika kituoni waliambiwa ameenda kununua peni.
Dereva alimwambia
haya twende ukachukue risiti yako muondoke na
watu wako. Dereva
aliingia na kupatiwa risiti kutoka kwenye kitabu kipya
ambacho kwa mujibu
wa dereva kilionekana dhahiri kuwa ni kipya.
Lakini kwa masaa
yote waliyokaa wanahabari kituoni hapo (takribani masaa
mawili),
hawakuwaona madereva wa magari waliokamatwa pamoja na gari lao
na kuandikiwa
makosa na faini pale Visiga, hawakufika Kituo cha Polisi
kupatiwa risiti,
kitendo ambacho kinaashiria fedha wanazolipishwa madereva
kwa kutenda makosa
hazitolewi risiti, hivyo mapato ya serikali kupotelea mifukoni mwa baadhi ya
askari wa kikosi cha usalama barabarani.
Baada ya
wanahabari hao kupata risiti majira ya saa 4:15 waliamua kuondoka kituoni hapo
kuanza safari ya kwenda Dodoma kuwahi msafara wa Katibu Mkuu wa CCM, Komredi
Abdulrahman Kinana uliokuwa unawasubiri kwenda Singida.
2 comments:
jipu hilo
Watatumbuliwa hao unacheza!
Post a Comment