Advertisements

Thursday, May 28, 2015

EXCLUSIVE: JOKATE ASUBIRIA MAAMUZI YA ALIKIBA



She was miss Tanzania namba two 2006 Jokate Mwegelo ambaye ni maarufu kwa jina la Kidoti, we know kwamba Jokate anavipaji vingi coz yeye ni Presenter, Actress, Fashionist, pia ni muimbaji wa muziki wa Bongo fleva.

Hivyo wakati Jokate akizungumza Exclusive na mwandishi wetu, alifungua ukurasa wa maelezo haya.

ABOUT FASHION
“Ilove Fashion coz nilitokea kwenye ulimbwende hapa nchini na Tasnia hii kiukweli bado haijafanyiwa vitu vingi,so kwangu mimi nifaraja kwa sababu Brand yangu ya Kidoti, imeweza kuchukua nafasi yake katika Tasnia hiyo in Tz”.

SIRI YA UREMBO WAKE

“Siri, kwanza huwa sikurupuki mara ninapotakiwa kuiweka ngozi yangu nyororo, huwa naenda kwa mtaalamu wa ngozi ananipatia ushauri na vyakula vya kutumia napendaga sana kumtumia Profesa masai ni mzuri sana kwenye masuala ya ngozi, mabli na hayo kuna vitu pia nimevigundua kama power foods, kunywa maji, kufanya mazoezi vinanisaidia sana”.



UTHUBUTU WAKE

“Unajua walimbende wengi huwa wanaingia kwenye mashindano pasipo kuwa na kusudio maalumu ndio maana baada ya shindano majina yao yanapotea. Lakini mimi niliingia coz nilikuwa nawaona kina Tedi Kalonga, Faraja Kota, Nancy nk so nilikuwa natamani kuingia ili nitimize malengo yangu hivyo nashukuru Mungu alinipa ujasili huo nikaweza kufanya vitu vingi kwa kujituma katika kile ninacho kitaka”.

MUZIKI WAKE

”Kipaji change cha muziki kilianzia kanisani nilikuwa naimba kwaya, hivyo kanisani tukawa tunapanga kutoa albam huku najiuliza nilini nitaweza kukaa na producer ni Record wimbo wangu? coz nilikuwa napenda sana kuona msanii anapeleka wimbo Radioni unahiti anapanda on the stage kuperform daah! Yaani hicho ndio kilicho nisukuma mimi kuingia kwenye muziki”.

MAPENZI YAKE

“Kuhusiana na uvumi wa mimi kudate na wakazi sikweli coz mimi na Wakazi ni marafiki ambao tulianza kujuana Tangu mimi nipo Chanell O, alikuwa anakuja Tanzania anataka mtu wa kumsaidia na kum-itroduce kwenye Industry. Mimi napenda sana mtu mwenye talents so ilipelekea mimi na wakazi tuka wa marafiki hadi hii leo lakini sio Wapenzi.

Now nipo Single ila kunamtu nampenda sijaamua tu coz bado tupo kwenye process, Alikiba he is a nice one, kuwanaye katika mahusiano ya kimapenzi hilo namuachia Mungu ila tutaangalia itakavyo kuwa mambo yakiwa sawa to Alikia itakuwa poa coz hayo ni maamuzi ya pande zote mbili”.

MUONO WAKE; DIAMOND Vs ALIKIBA

“Kiukweli nikikaa na Diamond ananifanya kuwa hasra lakini nikikaa na Alikiba ananifanya kutaka kuwa na muziki mzuriiii! Yaani anani ananiinspire sana,

Tangu niachane naye katika mapenzi yaani sina kitu nacho miss kwake, labda ucheshi ucheshi wake tu maana anachekesha, lakini sasa hivi namchukulia kama ndugu tu wa kawaida heshima vile yeah!”.

UJUMBE WAKE KWA FANS

“Nashukuru sana mashabiki wangu coz Mnanisapoti Mnanielewa Mnanipenda, kwa upendo wenu ndio maaana najitahidi kufanya vitu vizuri asanteni sana my fans nawapenda sana Mwaaaaaaa!”.
Credit:Team TZ

No comments: