Advertisements

Saturday, December 27, 2014

SHEREHE YA MIAKA 25 YA NDOA YA AMOS NA JESSICA MUSHALA IJUMAA DESEMBA 26, 2014

Amos na Jessica Mushala wakiwa meza kuu kusherehekea miaka 25 ya ndoa yao siku ya Ijumaa desemba 26, Lanham, Maryland nchini Marekani sherehe iliyokuwa na mambo mengi ya kumbukumbu ya maisha yao miaka 25 iliyopita.
Amos na Jessica Mushala wakiwa meza kuu na wapambe wao.
Wazee wa kimila wakiongozwa na Mzee Kasembe (kushoto)wakiwasubili Bi. Jessica Mushala na kundi lake kuingia ukumbini.
 Bi. Jessica Mushala na kundi lake wakiingia kwa mbwembwe zote ukumbini hapo.
Wazee wakimila wakiwa ukumbini

Kundi la kina mama waliomsindikiza Bi. Jessica Mushala wakiwa ukumbini.

Mchungaji akisoma neno kabla Bwn. Amos Mushala hajamvisha pete ya miaka 25 Bi. Jessica Mushala.

 Bwn. Amos Mushala akimvisha pete ya miaka 25 ya ndoa yao kama alama ya shukurani na kabla ya kufanya hivyo alitoa historia kidogo ya maisha na kuelezea ni kitu gani  kilichomvutia kutoka kwa Bi. Jessica Mushala na kupelekea kufunga ndoa nae miaka 25 iliyopita.

Wakina mama kundi la Jessica wakishuhudia Bi. Jessica Mushala akivishwa pete.
Wazee wa kimila nao wakipata ushuhuda.
Bi. Jessica Mushala akitoa shukurani zake kwa mumewe.
Densi ya kwanza ya miaka 25.
kwa picha zaidi bofya soma zaidi



4 comments:

Anonymous said...

Ujamaa Oyeee!!!! Sisi wabongo ni watu wa ajabu sana. Utasikia tu jana, juzi, n.k. eti fulani kafanya birthday bash, sherehe ya wedding anniversary ya miaka mitano, kumi, n.k. Sasa subiri msiba utokee Bongo; matanga dunia nzima!!! Street addresses na simu za wafiwa zinapelekwa duniani kote kukaribisha mkono wa pole! Lakini kwa sherehe, mh, ndugu na marafiki wa karibu tu ndo wanashikishwa! Huku ndiko kushikamana kwa raha na shida au kwa shida tu? Yumkini ujamaa wetu unakasoro kubwa!!!

Kaka Luke usibanie hii comment fadhali.

Anonymous said...

Hongereni saana.
Mwenyezi Mungu awaongezee mingine 50.

Salamu toka Bugandika omu Bagandika.
EILEMBE.

Unknown said...

Congratulations Jessica and Amos, May the good Lord give you many many more Blessed Healthy and Peaceful years to come.

Anonymous said...

safi sana wamefanya sherene ya kimila kama za kinigeria nilidhani movie hii.hongereni sana