Advertisements

Wednesday, September 17, 2014

MTOTO ALIYEZAMIA KWEYE NDEGE, ATOWEKA TENA NYUMBANI! SOMA ZAIDI HAPA!

Mtoto Happiness Rioba(10) aliyedaiwa kuzamia kwenye ndege kutoka Dar es Salaam kwenda Zanzibar bila kugundulika, ametoweka tena nyumbani kwao baada ya kukutanishwa na mama yake mzazi Sara Zefhania. 
Happiness ambaye ni mkazi wa eneo la Mkokozi, Wilaya ya Mkuranga mkoani Pwani inadaiwa ametoweka katika mazingira ya kutatanisha. 
Akizungumza na Mwananchi jana, Sara alisema mwanawe alitoweka jana saa sita mchana na kutokomea kusikojulikana.

Alisema asubuhi mtoto wake aliamka salama bila tatizo lolote na muda wote walikuwa pamoja kwa kuwa alikuwa na wageni kutoka kituo cha televisheni cha ITV, waliomuahadi kumtembelea nyumbani kwa lengo la kumuona Happiness.

“Aliamka vizuri tu na muda wote alikuwapo nyumbani, lakini ilipofika saa sita mchana, nilipigiwa simu na waandishi wa habari wa ITV kuwa nikawachukue katika kituo cha daladala... kabla sijaondoka nilimwambia mwanangu nakwenda kupokea wageni, lakini niporejea nyumbani na wageni hatukumkuta,” 

alisema Sara.
Alisema baada ya kumkosa alianza kumtafuta akishirikiana na waandishi hao pamoja na majirani, lakini hawakufanikiwa kumpata ndipo alipotoa taarifa kwa mjumbe wa Serikali za Mitaa na kuwataarifu ndugu, jamaa na marafiki.

Aidha, aliongeza mwanawe alipokuwa Zanzibar alifanya mambo ya ajabu likiwamo kuongea na paka, kula chakula kwa kutumia mkono wa kushoto, kutokuongea na watu pamoja na kutoweka katika mazingira ya kutatanisha.

1 comment:

Anonymous said...

Huyu mtoto anahitaji msaada wa kisaikolojia. Kuongea na wanyama inategemea kama maongezi ni njia moja au hao wanyama walimjibu. Hakuna ajabu kula na mkono wa kushoto. Badala ya kutengeneza mazingira ya kitamaduni, Mama Happy mpeleke mwanao kwa wataalamu wa saikoloji. Ukizidi kung'ang'ania maajabu wataalamu wa mambo ya kienyeji watasema amelogwa, basi na mwanao utampoteza. Swali kuu ni je Happy alisafiri vipi bila tiketi? SHirika la ndege wajibu hilo.