Advertisements

Thursday, April 25, 2024

TAADHARI IWE NGUZO KATIKA KIPINDI HIKI CHA MVUA NYINGI - KAMSAMBA


Na Issa Mwadangala
Wananchi wa Kata Mkulwa Tarafa ya Kamsamba Wilaya ya Momba Mkoani Songwe wametakiwa kuchukua tahadhari katika kipindi hiki cha mvua nyingi zinazoendelea kunyesha maeneo mbalimbali wilayani humo

Rai hiyo imetolewa Aprili 25,2024 na Mkuu wa Polisi Wilaya ya Momba Mrakibu Mwandamizi wa Polisi SSP Kennedy Msukwa wakati alipokuwa akitoa elimu juu ya madhara ya mvua nyingi zinazoendelea kunyesha maeneo mbalimbali wilayani humo.

SSP Msukwa amewataka wazazi na jamii kwa ujumla kuongeza umakini katika malezi ya watoto hasa katika kipindi hiki cha mvua nyingi zinazoendelea kunyesha ikiwa ni pamoja na kuwakataza kucheza michezo hatarishi kama kucheza na kuogelea kwenye maji yaliotuama (madimbwi) mabwawa na mito.
“Wazazi na walezi shughuli za kutafuta nguvu ya tumbo ziende sambamba na malezi ya watoto msiwaache watoto wajilee wenyewe kitendo ambacho kinapelekea watoto kusombwa na maji au kudumbukia kwenye mabwawa, mito na visimani kitendo hiki kinapunguza kizazi cha kesho ambacho ni hazina kwa taifa letu” alisema SSP Msukwa.

“Wavuvi mnatakiwa kufuata sharia na utaratibu wa shughuli zenu za kila siku ikiwa ni pamoja na kufanya uvuvi salama pia kuangalia hali ya hewa kabla ya kuingia kwenye shughuli zenu ili kujiepusha na madhara ambayo yanaweza kuepukika ikiwa ni pamoja na kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu pindi muonapo au mfanyiwapo kwa Jeshi la Polisi ili zishughulikiwe kwa haraka ili maeneo yenu yaendelee kuwa salama” alisisitiza SSP Msukwa.

PSPTB YAWAFIKIA WANACHUO WA CHUO CHA BAHARI DAR ES SALAAM



Mkuu wa Kitengo cha Masoko na Uhusiano kwa Umma ( PSPTB), Shamim Mdee akitoa maelezo kuhusu kazi zinazofanywa na Bodi hiyo wakati wa kutoa elimu kwa wanafunzi wa Astashada, Stashada na Shahada wanaosoma masomo ya Ununuzi katika Chuo cha Bahari Dar es Salaam (DMI) kilichopo jijini Dar es Salaam.

Bodi ya Wataalam wa Ununuzi na Ugavi (PSPTB) imetoa mafunzo Wanafunzi wa Shahada na Shahada ya Uzamili wanaosoma masomo ya Ununuzi katika Chuo cha Bahari Dar es Salaam (DMI) hii ikiwa ni mwendelezo wa kutoa elimu kwa umma hasa kwenye vyuo vinavyotoa masomo ya Ununuzi na Ugavi.
Akizungumza na Michuzi Blog, Mkuu wa Kitengo cha Masoko na Uhusiano kwa Umma ( PSPTB), Shamim Mdee amesema Bodi hiyo imeendelea kuwapa mafunzo Wanafunzi wa Vyuo mbalimbali wanaochukua kozi hiyo ya Ununuzi na Ugavi kuhusu shughuli zinazofanywa na Bodi, Usajili kwa njia ya mtandao pamoja na maadili na miiko ya taaluma hiyo.

Naye, Kaimu Mkuu wa Chuo, Taaluma, Utafiti na Ushauri Elekezi katika Chuo cha Bahari Dar es Salaam (DMI), Jonnes Lugoye ametoa shukrani kwa wafanyakazi wa PSPTB kwa kuweza kufika chuoni hapo kwa ajili ya kutoa elimu kuhusu kazi mbalimbali zinazofanywa na Bodi.
Kaimu Mkuu wa Chuo, Taaluma, Utafiti na Ushauri Elekezi - DMI, Jonnes Lugoye akiwakaribisha wageni kutoka Bodi ya Wataalam wa Ununuzi na Ugavi (PSPTB) walipofoka Chuo cha Bahari Dar es Salaam (DMI) kwa ajili ya kutoa elimu kuhusu Bodi hiyo.

MAKAMU WA RAIS DKT. MPANGO AMEWAAGIZA UCSAF KUENDELEA KUSIMAMIA UJENZI WA MINARA YA MAWASILIANO


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango akikata utepe kuashiria Uzinduzi wa Jengo la Ofisi ya Taasisi ya Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) lililopo eneo la Njedengwa mkoani Dodoma. Tarehe 25 Aprili 2024.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango akipokea zawadi kutoka kwa Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Nape Nnauye mara baada ya hafla ya Uzinduzi wa Jengo la Ofisi ya Taasisi ya Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) lililopo eneo la Njedengwa mkoani Dodoma. Tarehe 25 Aprili 2024.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango akiwa na Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Nape Nnauye, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Rosemary Senyamule,Mtendaji Mkuu wa UCSAF Justina Mashiba na viongozi mbalimbali katika picha ya pamoja watumishi wa Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) mara baada ya kuzindua jengo la Taasisi hiyo lililopo eneo la Njedengwa mkoani Dodoma. Tarehe 25 Aprili 2024.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango akihutubia wakati wa Uzinduzi wa Jengo la Ofisi ya Taasisi ya Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) lililopo eneo la Njedengwa mkoani Dodoma. Tarehe 25 Aprili 2024.

TUMIENI UZOEFU KUHARAKISHA MABADILIKO - BALOZI KUSILUKA


Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Dkt. Moses Kusiluka akiongea na Mabalozi katika warsha ya kutathimini utekelezaji wa Sera ya Mambo ya Nje inayofanyika mjini Kibaha, Pwani.
Kutoka Kushoto; Waziri wa Mambo ya Nje na Ushikiano wa Afrika Mashariki Mhe. January Makamba, Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Dkt. Moses, Naibu Waziri Mhe. Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk na Naibu Waziri anayeshughulikia masuala ya Afrika Mashariki Mhe. Stephen Byabato wakifuatilia warsha ya Mabalozi ya kutathimini utekelezaji wa Sera ya Mambo ya Nje inayofanyika katika Shule ya Uongozi ya Mwalimu Julius Nyerere mjini Kibaha, Pwani.

Mabalozi wamehimizwa kutumia taaluma, uzoefu na ujuzi tofauti waliokuwa nao kuharakisha mabadiliko ya kimfumo yanayoendelea ndani ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.

Kauli hiyo imetolewa  Aprili 23, 2024 na Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Dkt. Moses Kusiluka wakati anaongea na Mabalozi katika warsha ya siku 4 ya kutathimini utekelezaji wa Sera ya Mambo ya Nje inayofanyika mjini Kibaha tokea tarehe 21 Aprili 2024.

"Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki mmebarikiwa kuwa na watu wenye taaluma tofauti na wenye historia ya sekta tofauti, tumieni fursa yenu hii kumsadia Mwanadiplomasia namba moja, Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ambaye amewarahisishia kazi yenu kwa kuitekeleza diplomasia kwa vitendo", Balozi kusiluka alisema.

WAKUU WA SHULE, MADEREVA ZINGATIENI USALAMA WA WANAFUNZI KIPINDI CHA MVUA - MAJALIWA



WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewataka wamiliki wa shule na madereva wa mabasi yanayotoa huduma za usafiri kwa wanafunzi wajiridhishe kuhusu njia wanazopita ili kuhakikisha kunakuwepo na usalama wa wanafunzi wanaowabeba katika vyombo vya usafiri.

“Wazazi, Walezi na Jamii ya Watanzania kwa ujumla tushiriki kikamilifu katika kuhakikisha usalama wa wanafunzi wanapokwenda na kurudi Shuleni wakati wote hususan katika kipindi cha mvua.”

Kadhalika amesema kwa kuwa Serikali imetoa maelekezo ya kufunga shule zilizoathiriwa na mafuriko, halmashauri na wamiliki wa shule zisizo za Serikali waweke utaratibu wa kufidia muda wa vipindi ili kukamilisha kalenda ya muhula kama ilivyopangwa.

Ametoa wito huo leo (Alhamisi, Aprili 25, 2024) wakati akitoa taarifa ya serikali kuhusu changamoto za hali ya hewa bungeni jijini Dodoma.

Pia, amezitaka Taasisi za Serikali ziendelee, kukabiliana na maafa kwa kushirikiana na wadau kutekeleza majukumu yaliyoanishwa katika Mpango wa Kujiandaa na Kukabiliana na Madhara ya El-Nino pamoja na mipango ya kisekta ili kuzuia na kupunguza athari zinazoweza kujitokeza.

“Kamati za Maafa za Wilaya na Mikoa ziendelee kuchukua hatua stahiki ikiwemo kutoa tahadhari kwa wananchi na kusaidia wananchi kwa wakati pindi maafa yanapojitokeza.”

RC TANGA ATOA NENO KWA WANUNUZI WA ZAO LA MWANI


Mkuu wa Mkoa wa Tanga akizungumza wakati wa ziara ya kutembelea wakulima wa zao hilo katika Mtaa wa Sahare Kijijini Kata ya Mzingani Jijini Tanga ambao pia alizungumza na wakulima wa zao hilo kwenye wilaya za Tanga,Mkinga ,Muheza na Pangani ikiwa ni kuelekea Shamrashamra za kuelekea miaka 60 ya Muungano.
MKUU wa Mkoa wa Tanga Balozi Batilda Burian akitembea kuelekea baharini kuangalia kilimo cha Mwani wakati wa ziara yake ya kuwatembelea wakulima hao
MKUU wa Mkoa wa Tanga Balozi Batilda Burian akitoka kukagua zao la Mwani wakati wa ziara yake
Afisa Mfawidhi Idara ya Ukuzaji wa Viumbe Maji kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi Mkoa wa Tanga Omari Ally Mohamed akieleza jambo wakati wa ziara hiyo

TANZANIA NA CZECH MBIONI KUONDOA UTOZAJI WA KODI MARA MBILI


Naibu Katibu Mkuu wa Usimamizi wa Uchumi, Wizara ya Fedha Bw. Elijah Mwamdumbya na Mkurugenzi wa Ushirikiano wa Masuala ya Kodi Kimataifa wa Wizara ya Fedha ya Czech aliyeongoza ujumbe wa Czech Bw. Václav Zíka, wakisaini nyaraka za kukamilisha majadiliano, katika kikao kilichofanyika katika ukumbi wa Benki Kuu ya Tanzania jijini Dar es Salaam.
Naibu Katibu Mkuu wa Usimamizi wa Uchumi, Wizara ya Fedha Bw. Elijah Mwamdumbya na Mkurugenzi wa Ushirikiano wa Masuala ya Kodi Kimataifa wa Wizara ya Fedha ya Czech aliyeongoza ujumbe wa Czech Bw. Václav Zíka, wakibadilishana nyaraka za kukamilisha majadiliano, katika kikao kilichofanyika katika ukumbi wa Benki Kuu ya Tanzania jijini Dar es Salaam.
Naibu Katibu Mkuu wa Usimamizi wa Uchumi, Wizara ya Fedha Bw. Elijah Mwamdumbya na Mkurugenzi wa Ushirikiano wa Masuala ya Kodi Kimataifa wa Wizara ya Fedha ya Czech aliyeongoza ujumbe wa Czech Bw. Václav Zíka, wakionesha nyaraka za kukamilisha majadiliano, katika kikao kilichofanyika katika ukumbi wa Benki Kuu ya Tanzania jijini Dar es Salaam.
Naibu Katibu Mkuu wa Usimamizi wa Uchumi, Wizara ya Fedha Bw. Elijah Mwamdumbya na Mkurugenzi wa Ushirikiano wa Masuala ya Kodi Kimataifa wa Wizara ya Fedha ya Czech aliyeongoza ujumbe wa Czech Bw. Václav Zíka, wakiwa katika picha ya pamoja baada ya kukamilika kwa majadiliano ya kuondoa vikwazo vya kikodi katika kikao kilichofanyika katika ukumbi wa Benki Kuu ya Tanzania, jijini Dar es Salaam.
(Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Wizara ya Fedha)

DKT.DIMWA : ANENA JUU YA MUUNGANO

Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dkt.Mohamed Said Dimwa, akizungumza katika moja ya Mkutano wa CCM Zanzibar

NA IS-HAKA OMAR, ZANZIBAR.

NAIBU Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar Dkt. Mohamed Said Dimwa, amesema chama hicho kinaridhishwa na juhudi za Serikali zote mbili katika kuimarisha Muungano wa Tanganyika na Zanzibar.

Alisema muungano huo unaendelea kuvunja rekodi ya kudumu kwa miaka mingi zaidi ya miungano ya nchi nyingine barani Afrika na duniani kwa ujumla, kutokana na dhamira ya dhati ya kuasisiwa kwake.

Dkt Dimwa aliyasema hayo alipokuwa akizungumza katika mahojiano maalumu, ambapo amesema juhudi hizo zimeleta Mapinduzi ya kiuchumi,kiuchumi,kijamii na kuimarisha diplomasia ya kikanda na kimataifa.

Alifafanua kuwa Muungano huo ulioasisiwa Aprili 26, 1964 na hayati baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere na hayati Abeid Amani Karuma, umetimiza miaka 60 ukiwa na mafanikio ya wazi yanayozinufaisha nchi zote mbili Zanzibar na Tanzania Bara.

Alisema kuimarika kwa Muungano huo ni kutokana na mchango wa Viongozi wa awamu mbalimbali katika Serikali ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa kusimamia, kudumisha na kuimarisha umoja, amani na mshikamano.

TAKUKURU YAFANIKISHA MAREJESHO YA SH.MILIONI 439.2 KUTOKA KWA WANUFAIKA WA MIKOPO ASILIMIA 10 JIJI LA TANGA


Kamanda wa Takukuru Mkoa wa Tanga Victor Swella akizungumza na waandshi wa habari ambao hawapo pichani wakati akitoa taarifa ya utendaji kazi kwa kipindi cha Januari hadi Machi 2024 ambapo alisema kwamba moja ya kazi walioifanya ni ufuatiliaji wa ufanisi katika utekelezaji mkakati wa utoaji wa mikopo ya asilimia 10 kwa vijana,wanawake na watu wenye ulemavu.

Kamanda wa Takukuru Mkoa wa Tanga Victor Swella akizungumza na waandshi wa habari ambao hawapo pichani wakati akitoa taarifa ya utendaji kazi kwa kipindi cha Januari hadi Machi 2024 ambapo alisema kwamba moja ya kazi walioifanya ni ufuatiliaji wa ufanisi katika utekelezaji mkakati wa utoaji wa mikopo ya asilimia 10 kwa vijana,wanawake na watu wenye ulemavu.

Na Oscar Assenga,TANGA.
TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Takukuru Mkoani Tanga imefanikisha marejesho ya kiasi cha Sh. Milioni 439,279,300.00 kutoka kwa wanufaika wa mikopo asilimia 10 katika Halmashauri ya Jiji la Tanga.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Kamanda wa Takukuru Mkoa wa Tanga Victor Swella wakati akitoa taarifa ya utendaji kazi kwaa kipindi cha Januari hadi Machi 2024 ambapo alisema kwamba moja ya kazi walioifanya ni ufuatiliaji wa ufanisi katika utekelezaji mkakati wa utoaji wa mikopo ya asilimia 10 kwa vijana,wanawake na watu wenye ulemavu.

WANACHAMA WA TUGHE TAWI LA TCAA WAFANYA MKUTANO WA MWAKA MKOANI MOROGORO


Mkurugenzi wa Sheria  kutoka Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) Maria Makalla akizungumza wakati wa kufungua mkutano mkuu wa mwaka wa cha Chama cha Wafanyakazi wa Serikali kuu na Afya (TUGHE) Tawi la Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) uliofanyika Mkoani Morogoro
Mwenyekiti wa TUGHE Tawi la Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA), Bi. Jackline Ngoda akizungumza kuhusu namna wanavyoshirikiana na viongozi wa TCAA pamoja na kumkaribisha Mgeni rasmi.
Katibu wa TUGHE Mkoa wa Dar es Salaam Bi. Sara Rwezaula akitoa salamu za TUGHE Mkoa wa Dar es Salaam  wakati wa ufunguzi wa mkutano mkuu wa mwaka wa cha Chama cha Wafanyakazi wa Serikali kuu na Afya (TUGHE) Tawi la Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) uliofanyika Mkoani Morogoro.
Katibu wa TUGHE Tawi la Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA),Bw. Shukuru Mhina akifanywa utambulisho wa wajumbe wa mkutano mkuu wa mwaka wa TUGHE tawi la TCAA kwa Mgeni rasmi.

TASAF YATUMIA RUZUKU YA BILIONI 800 TANZANIA BARA NA VISIWANI KWA AJILI YA WALENGWA WA KAYA MASIKINI


Mkurugenzi wa Miradi – Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) Bw. John Steven.

Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) katika kipindi cha awamu ya pili ya utekelezaji iliyoanza mwaka 2020 umefanikiwa kutoa ruzuku ya zaidi ya shilingi bilioni 800 Tanzania bara na visiwani na kufanikiwa kuimarisha kiuchumi wa kaya maskini katika kuhakikisha wanapiga hatua katika maendeleo.

Akizungumza leo Aprili 24, 2024 katika Maonesho ya Maadhimisho ya miaka 60 ya Muungano yanayofanyika kwenye Viwanja vya Mnazi Mmoja, Dar es Salaam, Mkurugenzi wa Miradi – Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) Bw. John Steven, amesema kuwa walengwa wamefanikiwa kuimarika kiuchumi na kuweza kusaidia familia zao ikiwemo kusomesha na kujenga nyumba.

Bw. Steven amesema kuwa katika utekelezaji wa majukumu yao kwa sasa wametoa ruzuku shilingi bilioni 17.5 kwa halmashauri mbalimbali Tanzania Bara na Visiwani katika maeneo ya utekelezaji 35, huku maeneo 18 yakiwa katika mchakato wa utekelezaji.

“Miongoni mwa majukumu yetu ni kuunda vikundi ili wanachana waweze kujitegemea, pia kutoa ruzuku ya uzalishaji ambapo ni eneo jipya; TASAF imeanza kutekeleza kwa awamu ya pili ya Mpango Kunusuru Kaya za Walengwa“, amesema Bw. Steven.

Amefafanua kuwa wanachama wanaofanya vizuri katika vikundi wanapewa fedha wastani wa shilingi 350,000 kwa ajili ya kuongeza mtaji katika biashara ambazo tayari wameanza kufanya“, amesema Bw. Steven.

Wednesday, April 24, 2024

KAMISHNA JENERALI WA MAGEREZA ATUNUKIWA NA RAIS NISHANI YA KUMBUKUMBU YA MIAKA 60 YA MUUNGANO WA TANZANIA, LEO IKULU CHAMWINO, DODOMA

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan amemvalisha nishani ya Kumbukumbu ya miaka 60 ya Muungano Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza Mzee Ramadhani Nyamka leo Aprili 24, 2024 Ikulu chamwino Jijini Dodoma

SERIKALI YAZITAKA TAASISI ZA FEDHA ZA KUTOA MIKOPO KUFUATA UTARATIBU


Naibu Waziri wa Fedha Mhe. Hamad Hassan Chande (Mb) akijibu swali bungeni jijini Dodoma la Mheshimiwa Felista Deogratius Njau, Mbunge Viti Maalum aliyetaka kufahamu hatua zinazochukuliwa na Serikali kwa Taasisi za Fedha zinatoa mikopo yenye riba kubwa kinyume na muongozo wa BoT.

Na. Josephine Majura, WF, Dodoma
Serikali imesema kuwa inaendelea kuchukua hatua mbalimbali za kisera, kiutawala na kisheria ili kudhibiti tabia ya baadhi ya taasisi za fedha kutoa mikopo kinyume na miongozo iliyopo.

Hayo yameelezwa bungeni, jijini Dodoma na Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Hamad Hassan Chande (Mb), alipokuwa akijibu swali la Mheshimiwa Felista Deogratius Njau, Mbunge Viti Maalum aliyetaka kufahamu hatua zinazochukuliwa na Serikali kwa Taasisi za Fedha zinatoa mikopo yenye riba kubwa kinyume na muongozo wa BoT.

Mhe Chande, alisema kuwa Serikali imekuwa ikiendelea kusimamia utekelezaji wa Sera ya Fedha inayolenga kusimamia ukwasi katika mfumo wa kibenki ili kuendana na mahitaji halisi ya kiuchumi na kuweka mazingira rafiki ya utoaji mikopo.

“Serikali imekuwa ikiendelea kuhimiza benki kuwasilisha taarifa za wakopaji pamoja na kutumia kanzidata ya taarifa za wakopaji (credit reference bureau) wakati wa uchambuzi wa maombi ya mikopo ili kupunguza vihatarishi vya ongezeko la mikopo chechefu”, alisema Mhe. Chande.

WATUMISHI WIZARA YA FEDHA WATAKIWA KUENDELEA KUZINGATIA SHERIA


Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, Dkt. Natu El - Maamry Mwamba, akizungumza kuhusu watumishi kuendelea kufuata Sheria na Misingi ya Utawala Bora, wakati akifungua mkutano wa 37 wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara ya Fedha uliofanyika katika ukumbi wa Benki Kuu ya Tanzania, jijini Dar es Salaam.

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha Bi.Jenifa Omolo akiwataka watumishi wa Wizara kutoa maoni yao yatakayosaidia katika kuboresha utendaji wakati wa mkutano wa 37 wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara ya Fedha uliofanyika katika ukumbi wa Benki Kuu ya Tanzania, jijini Dar es Salaam.
Meza kuu ikiongozwa na Katibu Mkuu Wizara ya Fedha Dkt. Natu El Maamry Mwamba, wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wajumbe wa mkutano wa 37 wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara ya Fedha uliofanyika katika ukumbi wa Benki Kuu ya Tanzania, jijini Dar es Salaam. Kulia ni Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha Bi. Jenifa Omolo, Mkaguzi wa Ndani Mkuu wa Serikali, Bw. Benjamin Magai na Naibu Katibu Mkuu TUGHE Taifa Bw. Regemalila Rutatina. Kutoka kushoto ni, Mwenyekiti wa Baraza la Wafanyakazi Wizara ya Fedha Bi. Scholastica Okudo, Katibu wa Baraza la Wafanyakazi Bw. Tumwesige Kazura, Mhasibu Mkuu wa Serikali Bw. Leonard Mkude
Baadhi ya Wajumbe wa mkutano wa 37 wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara ya Fedha, wakifuatilia mawasilisho mbalimbali wakati wa mkutano huo uliofanyika katika ukumbi wa Benki Kuu ya Tanzania, jijini Dar es Salaam.

KATIBU MKUU, CCM AWAPONGEZA MABALOZI WAKIKAMILISHA WARSHA YA SIKU 4 KIBAHA


Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Dkt. Emmanuel Nchimbi akizungumza na Mabalozi wa Tanzania wanaoshiriki warsha ya siku 4 katika Chuo cha Uongozi cha Mwalimu Julius Nyerere mjini Kibaha, Pwani.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. January Makamba akizungumza wakati akiongoza warsha ya siku 4 ya Mabalozi iliyofanyika katika Chuo cha Uongozi cha Mwalimu Julius Nyerere mjini Kibaha, Pwani.

UMEME KWENYE GRIDI YA TAIFA WAFIKIA MEGAWATI 2,138


Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Mhe. Dkt. Doto Biteko (Mb)wakati akiwasilisha bungeni Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati kwa Mwaka wa Fedha 2024/25 katika Mkutano wa Kumi na Tano Kikao cha Kumi na Tatu.
Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Mhe. Dkt. Doto Biteko (Mb), ameliambia bunge kuwa katika mwaka 2023/2024 kuwezo wa mitambo ya kufua umeme iliyounganishwa kwenye mfumo wa Gridi ya Taifa umepanda kutoka Megawati (MW) 1,872.1 na kufikia Megawati (MW) 2,138, sawa na ongezeko la asilimia 14.2%.

Mhe. Dkt. Biteko ameyasema hayo leo Aprili 24, 2024 wakati akiwasilisha bungeni Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati kwa Mwaka wa Fedha 2024/25 katika Mkutano wa Kumi na Tano Kikao cha Kumi na Tatu.

RAIS WA ZANZIBAR DKT. MWINYI AFUNGUA JENGO LA SKULI YA SEKONDARI YA KIWANI PEMBA


RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akiwa na Mkewe Mama Mariam Mwinyi na (kushoto) Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Mhe. Ali Abdulgulam Hussein wakiondoa pazia kuashiria kuweka Jiwe la Msingi la Ufunguzi wa Jengo la Skuli ya Sekondari Kiwani Wilaya ya Mkoani Pemba, ikiwa ni shamrashamra za Maadhimisho ya sherehe za Miaka 60 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akiwa na Mkewe Mama Mariam Mwinyi na Viongozi wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar, wakisome maelezo ya Jiwe la Msingi la Ufunguzi wa Skuli ya Sekondari Kiwani, baada ya kukamilika ujenzi wake, ikiwa shamrashamra za sherehe za Maadhimisho ya Miaka 60 ya Muungano wa Tannganyika na Zanzibar,ufunguzi huo iliofanyika  23-4-2024
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akikata utepe kuifungua Skuli ya Sekondari Kiwani Wilaya ya Mkoani Pemba na (kushoto kwa Rais) Mke wa Zanzibar Mama Mariam Mwinyi na (kulia kwa Rais) Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Mhe. Ali Abdulgulam Hussein na Mkuu wa Mkoa wa Kusini Pemba Mhe. Mattar Zahor Masoud, wakati wa shamrashamra za sherehe za Maadhimisho ya Miaka 60 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar.
Muonekano wa Jengo Jipya la Skuli ya Sekondari Kiwani lililojengwa na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar na kufunguliwa leo 23-4-2024 na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi, ikiwa ni shamrashamra za Maadhimisho ya Miaka 60 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar.

RAIS SAMIA SULUHU HASSAN ATUNUKU NISHANI VIONGOZI MBALIMBALI


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akimtunuku na kumvalisha Nishani ya Mwenge wa Uhuru Daraja la Pili Waziri Mkuu Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Serikali ya Awamu ya Tatu Mhe. Fredrick kwenye hafla iliyofanyika katika Ikulu ya Chamwino Mkoani Dodoma tarehe 24 Aprili, 2024.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akimtunuku na kumvalisha Nishani ya Mwenge wa Uhuru Daraja la Pili Makamu Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mohamed Gharib Bilal kwenye hafla iliyofanyika katika Ikulu ya Chamwino Mkoani Dodoma tarehe 24 Aprili, 2024.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akimtunuku na kumvalisha Nishani ya Mwenge wa Uhuru Daraja la Pili Makamu wa Kwanza wa Rais na Waziri Mkuu Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. John Samwel Malecela kwenye hafla iliyofanyika katika Ikulu ya Chamwino Mkoani Dodoma tarehe 24 Aprili, 2024.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akimkabidhi Mama Janeth Magufuli Nishani ya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere ambayo aliipokea kwa niaba ya Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Serikali ya Awamu ya Tano Hayati Dkt. John Pombe Magufuli kwenye hafla iliyofanyika katika Ikulu ya Chamwino Mkoani Dodoma tarehe 24 Aprili, 2024. Nishani ya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere hutunukiwa kwa Wakuu wa Nchi Wastaafu (hai au marehemu) wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania walioingia madarakani kwa njia ya kikatiba na wameendelea kuonesha Maadili mema yenye nidhamu, heshima na mfano wa kuigwa.

WAKUU WA WILAYA TATU ZA MKOA WA KILIMANJARO WAKABIDHIWA MAGARI MAPYA


Na WILLIUM PAUL, MOSHI.
MKUU wa Mkoa wa Kilimanjaro, Nurdin Babu amekabidhi magari matatu kwa ajili ya wakuu wa wilaya za Rombo, Mwanga na Same ili kuongeza ufanisi wa utendaji na kuleta maendeleo ya mkoa yenye thamani ya zaidi ya milioni 200.

Akizungumza katika hafla fupi ya makabidhiano hayo nje ya viwanja wa ofisi za mkuu wa mkoa, Babu amesema Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ameanza kutekeleza maombi mbalimbali ya mkoa wa Kilimanjaro ya kuwapatia Wakuu wa wilaya vitendea kazi.

Babu alisema kuwa, Wabunge wamekuwa wakilalamika Bungeni kuhusiana na wakuu wa wilaya kukosa magari ambapo mkoa ulipanga kuhakikisha bajeti ya mwaka wa fedha 2023/24 mpaka ifikapo mwezi Juni mwaka huu wawe wameshanunua magari matatu ya wakuu wa wilaya.
Mkuu huyo wa Mkoa alisema kuwa, magari hayo yatatumika kwa ajili ya shughuli za kiserikali na kuwataka kwenda kuyatunza magari hayo kwani yamenunuliwa kwa gharama.